FILM TRAILER CLOUDS 112 (DR MAX)

NEW VIDEO FREDRIGO - NAJIULIZA

Saturday, November 9, 2013

HIZI NDIO SIMU MPYA ZA iPHONE ZINAZOWEZA KUPIMA JOTO RIDI

Posted by WaChAfU INC  
Tagged as:
2:58 AM

posted by TimeFm
Inder Singh ameutumia ugonjwa wake wa ini kama fursa ya kugundua kitu kipya na kikubwa katika dunia hii, ambapo sasa toleo jipya la simu aina ya iPhone halitatumika tu kutoa taarifa za kibenk, kutuma na kupokea pesa ama kuperuzi mitandao.
Ugunduzi wa Inder Singh unaiwezesha simu aina ya iPhone (toleo jipya) kuweza kutumika kupima jotoridi la mwili kama kipimajoto cha hospitali (thermometer) na hivyo kuwawezesha wazazi kujua afya za watoto wao mapema wakiwa nyumbani kwa kutumia simu.
Kipima joto maalum kitapachikwa kwenye iPhone hivyo kuiwezesha simu hiyo kupima jotoridi na kuonesha matokeo kwenye screen, ikiwa ni  pamoja na dalili za ugonjwa kwa mtumiaji.
Kwa hali hiyo inawezesha sio tu kuangalia afya wakati unapima, lakini pia kutunza record ya afya na inaweza kueleza kama unaweza kuwa na homa katika kipindi kifupi kijacho.
Inder Singh ambae aligundua kipima joto hicho maalum wakati akiwa anasumbuliwa na ugonjwa wa ini hivyo kutaka kufahamu afya yake kwa urahisi zaidi, amesema homa ni dalili ya magonjwa mengi hivyo kufahamu jotoridi la mwili kutasaidi watumiaji kufahamu afya zao kabla hawajashambuliwa zaidi na magonjwa.
“Fever is an early sign of illness and I wanted to revolutionise the world's most common medical device.”


TUMIA FACEBOOK KUTOA COMMENT HAPA:


Bofya like hapa show love:

KHAMIS HK (Writer)

My Phone Number :+255718109106,

  • My TWITTER
  • My FACEBOOK

  • 0 comments:

    Proudly Powered by Blogger.
    back to top